Published: OCTOBER 27, 2022 DOWNLOAD

The Tanzanian civil society hosted a 2-day Tanzanian PreCOP27-conference to ensure that local voices, needs and stories are represented and amplified during the upcoming climate conference COP27 in Egypt. The upcoming COP27 in November has to be an African-focused climate conference that centres around African priorities and ad-dress urgently needed issues as Loss & Damage, Adaptation, Health and Climate Finance. Climate action need to be informed by bottom-up and on-field experience of vulnerable communities. The Pre-COP27 strengthened and em-powered African voices to focus African issues in-scope of COP27.

Learn in this Press Release on Swahili about the priorities of Tanzanian Civil Society for COP27.

MSIMAMO WA AZAKI NA WAWAKILISHI WA JAMII KUELEKEA MKUTANO WA KIMATAIFA WA 27 DHIDI YA MABADILIKO YA TABIANCHI WA UNFCCC.


Kila mwaka nchi wanachama wa Umoja wa mataifa hukutana kujadiliana na kuweka mikakati mbalimbali ya kudhibiti na kukabiliana na masuala mazima ya mabadiliko ya tabianchi. Tanzania kama mwanachama wa umoja wa mataifa chini ya mwamvuli wa mkutano wa umoja wa mataifa wa mabadiliko ya tabianchi hushiriki mikutano hii ikiwa na uwakilishi kutoka ofisi ya makamu wa raisi kitengo cha mazingira kama wawakilishi wakuu wa nchi, wizara mbalimbali, na azaki zinazofanya kazi katika uchechemuzi wa masuala ya mazingira, maliasili na mabadiliko ya tabianchi.

 

Mwaka huu, mkutano huu unatarajiwa kufanyika Misri kuanzia tarehe 6/11/2022 mpaka 18/11/2022. Dhima kubwa ya mkutano huu ni kujadiliana ukamilishaji na utekelezaji wa mkataba wa Paris wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ikiwa pia kuweka uwekezaji na utoaji wa pesa katika nyezo/njia zinazo dhibiti uzalishaji wa gesi joto.

 

Tanzania inautamaduni wa kukutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali kujadiliana na kutengeneza msimamo moja ya nchi ambayo itaongoza wawakilishi wa Tanzania katika mkutano huu wa majadiliano na kuhakikisha maslahi ya nchi yanazingatiwa katika kuhakikisha uwezo na fursa za udhibiti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Mwaka huu  azaki za CAN Tanzania, FORUMCC, ActionAid, Save the Children na PINGOs Forum kwa ufadhili wa Uk-Aid, FES Tanzania na Preston Werner Ventures, wameandaa mkutano wa maandalizi kueleke mkutano mkubwa utakaofanyika Sharm el Sheikh,Misri. Mkutano huu umekutanisha wawakilishi wa azaki, vyama vya wafanyakazi, vijana, watoto, wakulima, wafugaji, na wavuvi.

 

Hoja kubwa ambayo wadau wanajadiliana na kutoa msimamo wa kuzingatiwa katika mkutano wa COP27 ni zifuatazo;

       Mchango wa Tanzania katika uzalishaji wa gesi joto ni mdogo sana, na jamii ya Tanzania inaathirika kwa kiwango kikubwa na athari za mabadiliko ya tabianchi. Kipaumbele cha jamii ya Tanzania ni kwenye kuwezesha ustahimilivu wa athari za mabadiliko ya tabianchi na pamoja na kutoa ahueni ya hasara na uharibifu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

       Tunasisitiza utoaji wa fedha kuhakikisha uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kupata nafuu na ahueni kutokana na hasara na uharibifu unaosababishwa na majanga yanayochagizwa na mabadiliko ya tabianchi. Tunahitaji mifumo na michakato ya kuwezesha upatikanaji wa fedha hizi kuwekwa vizuri na kuhakikisha upatikanaji wa moja kwa moja wa fedha hizi.

       Tunasisitiza udhibiti wa uzalishaji wa gesi joto kwa nchi zilizoendelea kwa kuongeza nia zao pamoja na kuwezesha ufyonzaji wa gesi joto, ili kupunguza madhara na athari za mabadiliko ya tabianchi. uharibifu na upoteaji wa mali inayosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi, pamoja na kuhimiza ukamilishaji wa mkataba wa Paris.

       Tunakataza ushawishi na uletaji wa nyenzo, teknolojia na suluhisho zenye lebo ya ukabilianaji na athari za mabadiliko ya tabianchi ambazo ni za uongo zisizo na tija katika utunzaji wa mazingira, zinazodidimiza maendeleo na zinazo jenga utegemezi kwa nchi zinazoendelea.

       Tunakataza siasa chafu zenye lengo la kuchelewesha utekelezaji wa mkataba wa Paris na zenye kunufaisha wazalishaji wakubwa wa gesi joto katika mkutano huu. Badala yake, tunasisitiza kuangalia zaidi masuala yatakayo ongeza ustahimilivu na udhibiti wa mabadiliko ya tabianchi

       Tunasisitiza uhitaji wa kujengewa uwezo na kupatiwa teknolojia ili kuwezesha ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuwezesha hatua shahiki za kupunguza athari na uharibifu unaochagizwa na mabadiliko ya tabianchi

       Tunahitaji wawakilishi wetu kutoka Africa na kwenye makundi ya pamoja kuwa na umoja na kusimamia hoja za msingi za maendeleo ambazo zinazingatia uwezo na haja za jamii zilizo na mazingira magumu kustahimili athari za mabadiliko ya tabianchi

       Tunasikitishwa na upungufu wa kila mwaka wa uwakilishi na ushiriki wa azaki na wawakilishi wa jamii katika Mikutano hii, kupitia utoaji wa nafasi chache za ushiriki, uzuiaji wa kushiriki ndani ya vyumba vya mkutano na vikwazo vingi kwenye utoaji visa kwa wenyeji wa mikutano. Tunahitaji nafasi nyingi za uwakilishi kutoka kwenye jamii zetu ili kuhakikisha mslahi na misimamo yetu inazingatiwa.